Tuesday, February 10, 2015

JIHAD YA NAFSI

MAPAMBANO DHIDI YA NAFSI YAKO

Roho ya binadamu ni eneo la mapambano ya nguvu mbili za mashindano. Nguvu ya Mungu humvutia mtu kwenye nyanja ya mbinguni, na kumhamasisha kwenye matendo ya wema. Nguvu za kishetani humshawishi kuelekea maeneo ya giza na aibu, na kumualika kwenye matendo maovu. Wakati nguvu ya Mungu ni ushindi, mtu anaibuka kuwa mwema na mpole, kwenye ufuasi wa Mtume (S), watu wa Mungu, na wacha Mungu. Wakati, hata hivyo, vikosi vya kishetani hutawala, mtu anakuwa muasi na muovu na kuwa katika kundi pamoja na makafiri, madhalimu, watenda maovu na wale ambao wamelaaniwa.

""Na kwa nafsi na kuilinganisha kwake! Akaifahamisha uovuna takua yake. Hakika amefaulu aliyeitakasa (Qur'an, 91: 7-9)""

MANENO YA MTUME(S.A.W)

""Imam Ja'far al-Sadiq (as) amesema: "Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad(s) alipeleka kikosi cha jeshi (kwenye uwanja wa mapambano). Walipata ushindi wakati waliporudi kwao, yeye Mtume (s) alisema: '. Heri yao wale ambao walifanya jihadi ndogo na bado kufanya jihadi kubwa' Wakati alipoulizwa, 'Ni ipi Jihad kubwa? Mtume (s.a.w.w) akasema : 'jihadi ya nafsi (mapambano dhidi ya wewe mwenyewe)' ".[Al-Majlisi, Bihar al-Anwar, Juzuu ya 19, uk. 182, hadith namba. 31]""

USHAURI KATIKA MAPAMBANO YA NAFSI YAKO
  1. Ni asili ya binadamu kumshukuru mwingine ambaye amekuwa mwema.Tafakari na kadiria zile fadhila za dhahiri na za siri alizotupa Mwenyezi juu yetu.Viumbe wote wa Mungu hawawezi hata kutoa sehemu ya fadhila hizo.

  2. Angalia hewa tunayopumua sisi mchana na usiku, na juu ya maisha yetu ambayo pia ile ya viumbe hai wengine ni tegemezi. Hakuna kinachoweza kubakia hai kama kikinyimwa hewa hata kwa dakika chache. Ni vipi zawadi hii ya ajabu ya Mungu! Kama watu wote wa ulimwengu wataungana pamoja kwa kazi hii, hawataweza kuunda zawadi hii, hawataweza kufanya hivyo. Katika njia hiyo hiyo, tafakari juu ya karama zingine za Mungu kama vile hisia za nje za mwili za kuona, kusikia, ladha, harufu, na kugusa, na uwezo wa ndani kama vile kufikiri, dhana, na kuhoji, kila mmoja ambaye amebeba faida zisizo na ukomo na ambazo zimetolewa kwetu na Bwana wetu. Mwenyezi Mungu Muumba na Mfalme wa ulimwengu huu. Binadamu, ni kiumbe aliyewekwa katika moja ya sayari ndogo, ameshindwa kabisa kufahamu kiwango kidogo cha dunia yake mwenyewe, jua ambalo hawezi hata kulilinganisha na sayari nyingine ya jua iliyoko mbali zaidi ya kundi la nyota. Mfumo wetu wa jua ni kitu kisicholinganishwa na mifumo kadhaa ya nishati ya jua, ambayo bado haijaepuka darubini yenye nguvu kubwa ya wapelelezi na wachunguzi. Angalia katika ubongo wa binadamu-ni kipi wanachovutia viumbe! Je, yawezekana binadamu kuunganisha jitihada zao na kuweza kufanya hata moja seli hai ya ubongo (kiini cha ubongo) ambayo Mwenyezi Mungu ameumba na ameiumba kwa wakati wote! Hakika hii akili tuliyopewa na Mungu inastahili kuwa kiti cha mawazo na maongozi mema tu, na wala sio mawazo mabaya!   ALLAH AALAM


0 comments:

Post a Comment

MWEZI WA MUHARRAAM NA UZUSHI

بسم الله الرحمن الرحيم MASHIA NA BIDAA ZA MWEZI WA MUHARRAMU. Mwezi wa Muharramu ni miongoni mwa miezi mitukufu kwa mujibu wa mafundis...