JIHADI ni neno lililopotoshwa maana yake kwa makusudi. Leo neno hilo limepoteza kabisa ile maana yake halisi. Maana ya jihadi imegeuzwa kuwa ni vita, umwagaji damu na ulipuaji mabomu! Hilo halikutokea kwa bahati mbaya. Ni mkakati maalumu ulioandaliwa namaadui, kwa lengo la kuudhofisha Uislamu.
Moja wapo ya hukmu za Kiislamu zinazopigwa vita kwa wingi na wamagharibi ni Jihad.Kwa kupitia vyombo vya habari wamagharibi wamefaulu kwa kiasi kikubwa kuchafua mabongo ya wasokuwa waislamu kuchukia Waislamu na Uislamu. Kumejengeka dhana mbovu kwa watu wengi wasojua Uislamu kuwa Waislamu ndio wachangiaji wa mauaji ya watu kote duniani kwani hao ni magaidi.Wamagharibi wameitungia jihadi jina jengine ‘vita vitakatifu’[Holy war] kueneza urongo dhidi yake na kuonyesha kwamba waislamu ndio wawauaji wakubwa na wao ndio chanzo kikubwa cha ukosefu wa usalama duniani. Kampeni hii imewafanya Waislamu wakiwemo mashekh kuanza kujisafisha kwenye vyombo vya habari kwa kupindisha hukmu ya Jihad na wengine kuanza kuomba samahani serikali hususan kunapotokea mashambulizi.Licha ya kuwa mashambulizi mengi yaitwayo ya kigaidi hutekelezwa na serikali kisha kusingiziwa Waislamu,wengi ya Waislamu wameshindwa kabisa kufafanua suala hili kwa sura yake halisi bali wamekuwa wakionekana kutupiana lawama.Hii ina maana kuwa tayari baadhi ya Waislamu wamekubali kuwa wao ni magaidi.
Jihadi iliwajenga Waislamu moyo wa ushujaa na ujasiri wa kutokubali kuonewa au kudhulumiwa. Walijitolea kwa hali na mali kuutetea Uislamu, kila pale zilipojitokeza dalili za kutaka kuhujumiwa. Watetezi hao ndo walioitwa Mujahidina. Cheo cha Mujahidina kilikuwa kina daraja bora, na kila Muislamu alitamani akifikie. Mtume (saw) alipoulizwa, "Mtu gani ni bora?" Alijibu, "ni muumini anayefanya juhudi katika njia ya Allah, kwa mali yake na nafsi yake", yaani "Mujahid".
Jihad ikawa ni tishio kwa maadui. Waligundua kuwa madamu Waislamu watadumu na moyo wa kujitolea kwa ajili ya jihadi, basi hawatashindwa na lolote. Wakaona hakuna njia ya kuudhofisha Uislamu na Waislamu wenyewe, isipokuwa ni kuifanya jihadi iwe ni chukizo nyoyoni mwa watu. Wakaanza tafsiri potofu ya neno hilo. Wakalitafsiri neno jihadi kwa maana ya vita vitakatifu. Wamefanya hivyo ili ionekane kuwa Uislamu ni dini ya vita na mauaji. Wakaufanya Uislamu ni dini iliyotumia nguvu kuwalazimisha watu waikubali. Wakachora katika akili za watu picha inayoonyesha kuwa jihadi ni vita vya kusaka makafiri na kuwaua. Na wanaposema Mujahidina hukusudiwa jeshi la watu waliovaa kanzu, waliopiga vilemba vichwani, waliofuga madevu mengi mengi, wanaofananafanana na Waarabu, au ‘Wamanga", kama walivyozoea kuwaita walioshika panga mikononi, wanaozunguka huku na kule kuua makafiri. Ndiyo maana hawaoni aibu kupaza sauti zao na kuutangazia ulimwengu, kuwa kuna makontena bandarini yanayotaka kutumiwa na Mujahidina kuchinjia makafiri. Na vyombo vya habari navyo bila ya kutafiti na kupata ithbati, tayari wanazishabikia habari hizo na kuzieneza.
Kwa vile panga na majambia si silaha tena katika zama hizi, basi sasa Mujahidina, moja kwa moja wanahusishwa na ulipuaji mabomu. Kila linapolipuka bomu wa mwanzo kushutumiwa huwa ni Mujahidina. Imejengwa dhana kuwa Waislamu tu ndio wakorofi wa kutega mabomu. Asiye Muislamu huonekana ni mstaarabu, na ni mtu mwenye upendo, hawezi kushiriki katika vitendo vya ugaidi hata kama ushahidi utaunyooshea kidole! Tokea lini ugaidi ukawa una dini, kabila au rangi?
Uislamu si dini ya mabavu. Uislamu unajali zaidi hoja na siyo nguvu. Unamtaka mwanadamu atumie akili yake katika kumtambua Muumba wake. Ndiyo ukaona Qur’an Tukufu haimlazimishi mtu kumkubali Mwenyezi Mungu bali inamtaka binadamu atumie akili kuzingatia Qur’an inasema: "Je! Hwawatazamia ngamia jinsi walivyoumbwa? Na mbingu jinsi zilivyoinuliwa. Na milima jinsi ilivyothubutishwa. Na ardhi jinsi ilivyotandazwa?" (Al- Ghashiyah 88:17-20).
Mwenyezi Mungu (sw) anawataka wanaadamu watazame umbo la ngamia, mbingu, majabali na ardhi, kisha watumie akili zao kupima ili waone kama vyote hivyo vimekuja vyenyewe hivi hivi au yuko aliyeviumba? Kisha Mwenyezi Mungu (sw) akamwambia Mtume wake, "Basi kumbusha, hakika wewe ni mkumbushaji (tu). Wewe si mwenye kuwatenza nguvu’. (Al-Ghashiyah 88:21-22)
Utaona Uislamu umeilenga zaidi akili ya mwanadamu. Mwanadamu amekuwa ni kiumbe bora kuliko mnyama kwa sababu ya akili aliyo nayo. Binadamu asiye na akili hatafautiani na mnyama. Mwenye akili hupima kila analoambiwa. Akiliona linakubaliana na akili analikubali na akigundua halikubaliani na akili, basi naye hulikataa. Na Uislamu ndivyo ulivyo. Hoja zake zinachuana na akili ya binadamu. Kama akili inakataa kukubali kuwa 1 + 1 + 1 ni 3, kwanini basi akili itaabishwe kwa kupewa jawabu isiyoridhia na ya uwongo?
Ukweli na uwazi umekuwa ndiyo silaha kubwa ya Uislamu. Na kwa silaha hiyo Uislamu umeweza kuwateka wengi sana. Baada ya kuonekana wengi wanasalimu amri mbele ya hoja za kweli za Uislamu wengine hawakuweza kulivulia hilo litendeke mbele ya macho yao.
Ndiyo wakavumbua kila aina ya kisingizio. Ati wahubiri wa Kiislamu wanazikashifu dini nyingine. Sheria ya nchi inamtaka mwenye kukashifiwa aende mbele ya vyombo vya sheria kushitaki. Lakini mpaka hivi leo, bado haijajitokeza madhehebu yoyote ya kidini kushitaki kuwa imekashifiwa, jambo ambalo linathibitisha kuwa hapana anayekashifiwa.
Na vipi Muislamu atakashifu dini nyingine na wakati Uislamu wenyewe unakataza kufanya hivyo.
Qur’an Tukufu inasema, "Wala msiwatukane wale ambao wanaabudu, kinyume cha Mwenyezi Mungu, wasije wakamtukana Mwenyezi Mungu kwa jeuri zao bila kujua". (Al An-Am 6:108). Na Mwenyezi Mungu (sw) alimwagiza Mtume wake kwa kumwambia, "Waite (watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora (siyo kwa kuwatukana wao au kutukana dini zao)". (An Nahl 16:125).
Mtume (saw) akafuata maagizo ya Mola wake. Kwa miaka 13 mfululizo aliwalingania watu wa Makka kwa maneno mema, hekima na busara. Katu hakuwatukana wala kutumia nguvu. Kinyume chake yeye na wafuasi wake ndio waliokuwa wakitukanwa, kunyanyaswa na kuteswa.
Na kila mara Mwenyezi Mungu akimwambia, "Basi wasamehe na uwaambie (maneno ya) salama (labda mwisho wake watatambua). Hivi karibuni watajua". (Az-Zukhruf 43:89).
Na pale alipofanyiwa uovu aliambiwa, "Ondosha mabaya (unayofanyiwa) kwa (kulipa) mema". (Al Muuminun 23:96). Hatimaye ilibidi Mtume (saw) na masahaba wake wakimbie Makka kusalimisha maisha yao.
Huenda mwulizaji akauliza itakuwaje isemwe kuwa Uislamu ni dini ya amani, na jihadi siyo vita na kumbe Waislamu walipigana vita vya jihadi? Swali hili ni zuri sana. Vita hupiganwa kwa malengo mawili makuu. Aidha kwa kupigania maslahi ya kidunia, kama kutaka kuziteka na kuzitawala nchi nyingine, kupata mali ghafi au masoko ya kuuzia bidhaa, au pia vita vinaweza kupiganwa kwa ajili ya kujilinda na mashambulizi ya adui.
Kwa vyovyote vile vita hivyo viwili havifanani. Vile vya aina ya kwanza ni vya uchokozi na vile vya pili ni vya kujihami. Uislamu unaviita vile vita vya uchokozi "Harbun" na vile vya kujihami "Jihadun".
Ilitarajiwa Waislamu wafanye nini baada ya kudhulumiwa uhuru wa kuabudu na kufukuzwa katika nchi yao? Iisitoshe na hata walipokimbilia Madina kama wakimbizi na kupewa hifadhi ya kisiasa huko bado waliandamwa na maadui na kushambuliwa.
Bila shaka hiyo ni jeuri iliyopindukia na hakuna atakayeivumilia. Ndipo hapo Mwenyezi Mungu (sw) akawapa Waislamu ruhusa ya kupigana. Ruhusa ya kwanza waliyopewa ilikuwa "Wameruhusiwa (kupigana) wale wanaopigwa, kwa sababu wamedhulumiwa. Na kwa yakini Mwenyezi Mungu ni muweza wa kuwasaidia ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki ila kwa sababu wanasema ‘Mola wetu ni Allah’ (Al Hajj 22:39-40)
Huo ukawa ndio mwanzo wa vita vya jihadi. Lakini msisitizo mkubwa waliowekewa ulikuwa wasipigane vita vya uvamizi bali vita vya kujihami. Na shahidi wa haya ni ile kauli ya Allah (sw) inayosema, "Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaokupigeni, wala msipindukie mipaka (mkawapiga wasiowapigeni). Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi warukao mipaka" (Al Baqarah 2:190).
Ukichunguza utaona kila lnapotajwa neno jihadi katika Qur’an Tukufu au katika hadithi za Mtume (saw) basi huongezwa Fiy Sabilil Lahi. Maana yake jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa ajili ya kuonyesha kuwa si lazima jihadi kila siku iwe ina maana ya vita.
Neno juhudi pamoja na kustahamili mashaka na taabu katika kufikia jihadi ni kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu kwa kustahili kila aina ya misukosuko inayoweza kumfika mtu.
Moja wapo ya hukmu za Kiislamu zinazopigwa vita kwa wingi na wamagharibi ni Jihad.Kwa kupitia vyombo vya habari wamagharibi wamefaulu kwa kiasi kikubwa kuchafua mabongo ya wasokuwa waislamu kuchukia Waislamu na Uislamu. Kumejengeka dhana mbovu kwa watu wengi wasojua Uislamu kuwa Waislamu ndio wachangiaji wa mauaji ya watu kote duniani kwani hao ni magaidi.Wamagharibi wameitungia jihadi jina jengine ‘vita vitakatifu’[Holy war] kueneza urongo dhidi yake na kuonyesha kwamba waislamu ndio wawauaji wakubwa na wao ndio chanzo kikubwa cha ukosefu wa usalama duniani. Kampeni hii imewafanya Waislamu wakiwemo mashekh kuanza kujisafisha kwenye vyombo vya habari kwa kupindisha hukmu ya Jihad na wengine kuanza kuomba samahani serikali hususan kunapotokea mashambulizi.Licha ya kuwa mashambulizi mengi yaitwayo ya kigaidi hutekelezwa na serikali kisha kusingiziwa Waislamu,wengi ya Waislamu wameshindwa kabisa kufafanua suala hili kwa sura yake halisi bali wamekuwa wakionekana kutupiana lawama.Hii ina maana kuwa tayari baadhi ya Waislamu wamekubali kuwa wao ni magaidi.
Jihadi iliwajenga Waislamu moyo wa ushujaa na ujasiri wa kutokubali kuonewa au kudhulumiwa. Walijitolea kwa hali na mali kuutetea Uislamu, kila pale zilipojitokeza dalili za kutaka kuhujumiwa. Watetezi hao ndo walioitwa Mujahidina. Cheo cha Mujahidina kilikuwa kina daraja bora, na kila Muislamu alitamani akifikie. Mtume (saw) alipoulizwa, "Mtu gani ni bora?" Alijibu, "ni muumini anayefanya juhudi katika njia ya Allah, kwa mali yake na nafsi yake", yaani "Mujahid".
Jihad ikawa ni tishio kwa maadui. Waligundua kuwa madamu Waislamu watadumu na moyo wa kujitolea kwa ajili ya jihadi, basi hawatashindwa na lolote. Wakaona hakuna njia ya kuudhofisha Uislamu na Waislamu wenyewe, isipokuwa ni kuifanya jihadi iwe ni chukizo nyoyoni mwa watu. Wakaanza tafsiri potofu ya neno hilo. Wakalitafsiri neno jihadi kwa maana ya vita vitakatifu. Wamefanya hivyo ili ionekane kuwa Uislamu ni dini ya vita na mauaji. Wakaufanya Uislamu ni dini iliyotumia nguvu kuwalazimisha watu waikubali. Wakachora katika akili za watu picha inayoonyesha kuwa jihadi ni vita vya kusaka makafiri na kuwaua. Na wanaposema Mujahidina hukusudiwa jeshi la watu waliovaa kanzu, waliopiga vilemba vichwani, waliofuga madevu mengi mengi, wanaofananafanana na Waarabu, au ‘Wamanga", kama walivyozoea kuwaita walioshika panga mikononi, wanaozunguka huku na kule kuua makafiri. Ndiyo maana hawaoni aibu kupaza sauti zao na kuutangazia ulimwengu, kuwa kuna makontena bandarini yanayotaka kutumiwa na Mujahidina kuchinjia makafiri. Na vyombo vya habari navyo bila ya kutafiti na kupata ithbati, tayari wanazishabikia habari hizo na kuzieneza.
Kwa vile panga na majambia si silaha tena katika zama hizi, basi sasa Mujahidina, moja kwa moja wanahusishwa na ulipuaji mabomu. Kila linapolipuka bomu wa mwanzo kushutumiwa huwa ni Mujahidina. Imejengwa dhana kuwa Waislamu tu ndio wakorofi wa kutega mabomu. Asiye Muislamu huonekana ni mstaarabu, na ni mtu mwenye upendo, hawezi kushiriki katika vitendo vya ugaidi hata kama ushahidi utaunyooshea kidole! Tokea lini ugaidi ukawa una dini, kabila au rangi?
Uislamu si dini ya mabavu. Uislamu unajali zaidi hoja na siyo nguvu. Unamtaka mwanadamu atumie akili yake katika kumtambua Muumba wake. Ndiyo ukaona Qur’an Tukufu haimlazimishi mtu kumkubali Mwenyezi Mungu bali inamtaka binadamu atumie akili kuzingatia Qur’an inasema: "Je! Hwawatazamia ngamia jinsi walivyoumbwa? Na mbingu jinsi zilivyoinuliwa. Na milima jinsi ilivyothubutishwa. Na ardhi jinsi ilivyotandazwa?" (Al- Ghashiyah 88:17-20).
Mwenyezi Mungu (sw) anawataka wanaadamu watazame umbo la ngamia, mbingu, majabali na ardhi, kisha watumie akili zao kupima ili waone kama vyote hivyo vimekuja vyenyewe hivi hivi au yuko aliyeviumba? Kisha Mwenyezi Mungu (sw) akamwambia Mtume wake, "Basi kumbusha, hakika wewe ni mkumbushaji (tu). Wewe si mwenye kuwatenza nguvu’. (Al-Ghashiyah 88:21-22)
Utaona Uislamu umeilenga zaidi akili ya mwanadamu. Mwanadamu amekuwa ni kiumbe bora kuliko mnyama kwa sababu ya akili aliyo nayo. Binadamu asiye na akili hatafautiani na mnyama. Mwenye akili hupima kila analoambiwa. Akiliona linakubaliana na akili analikubali na akigundua halikubaliani na akili, basi naye hulikataa. Na Uislamu ndivyo ulivyo. Hoja zake zinachuana na akili ya binadamu. Kama akili inakataa kukubali kuwa 1 + 1 + 1 ni 3, kwanini basi akili itaabishwe kwa kupewa jawabu isiyoridhia na ya uwongo?
Ukweli na uwazi umekuwa ndiyo silaha kubwa ya Uislamu. Na kwa silaha hiyo Uislamu umeweza kuwateka wengi sana. Baada ya kuonekana wengi wanasalimu amri mbele ya hoja za kweli za Uislamu wengine hawakuweza kulivulia hilo litendeke mbele ya macho yao.
Ndiyo wakavumbua kila aina ya kisingizio. Ati wahubiri wa Kiislamu wanazikashifu dini nyingine. Sheria ya nchi inamtaka mwenye kukashifiwa aende mbele ya vyombo vya sheria kushitaki. Lakini mpaka hivi leo, bado haijajitokeza madhehebu yoyote ya kidini kushitaki kuwa imekashifiwa, jambo ambalo linathibitisha kuwa hapana anayekashifiwa.
Na vipi Muislamu atakashifu dini nyingine na wakati Uislamu wenyewe unakataza kufanya hivyo.
Qur’an Tukufu inasema, "Wala msiwatukane wale ambao wanaabudu, kinyume cha Mwenyezi Mungu, wasije wakamtukana Mwenyezi Mungu kwa jeuri zao bila kujua". (Al An-Am 6:108). Na Mwenyezi Mungu (sw) alimwagiza Mtume wake kwa kumwambia, "Waite (watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora (siyo kwa kuwatukana wao au kutukana dini zao)". (An Nahl 16:125).
Mtume (saw) akafuata maagizo ya Mola wake. Kwa miaka 13 mfululizo aliwalingania watu wa Makka kwa maneno mema, hekima na busara. Katu hakuwatukana wala kutumia nguvu. Kinyume chake yeye na wafuasi wake ndio waliokuwa wakitukanwa, kunyanyaswa na kuteswa.
Na kila mara Mwenyezi Mungu akimwambia, "Basi wasamehe na uwaambie (maneno ya) salama (labda mwisho wake watatambua). Hivi karibuni watajua". (Az-Zukhruf 43:89).
Na pale alipofanyiwa uovu aliambiwa, "Ondosha mabaya (unayofanyiwa) kwa (kulipa) mema". (Al Muuminun 23:96). Hatimaye ilibidi Mtume (saw) na masahaba wake wakimbie Makka kusalimisha maisha yao.
Huenda mwulizaji akauliza itakuwaje isemwe kuwa Uislamu ni dini ya amani, na jihadi siyo vita na kumbe Waislamu walipigana vita vya jihadi? Swali hili ni zuri sana. Vita hupiganwa kwa malengo mawili makuu. Aidha kwa kupigania maslahi ya kidunia, kama kutaka kuziteka na kuzitawala nchi nyingine, kupata mali ghafi au masoko ya kuuzia bidhaa, au pia vita vinaweza kupiganwa kwa ajili ya kujilinda na mashambulizi ya adui.
Kwa vyovyote vile vita hivyo viwili havifanani. Vile vya aina ya kwanza ni vya uchokozi na vile vya pili ni vya kujihami. Uislamu unaviita vile vita vya uchokozi "Harbun" na vile vya kujihami "Jihadun".
Ilitarajiwa Waislamu wafanye nini baada ya kudhulumiwa uhuru wa kuabudu na kufukuzwa katika nchi yao? Iisitoshe na hata walipokimbilia Madina kama wakimbizi na kupewa hifadhi ya kisiasa huko bado waliandamwa na maadui na kushambuliwa.
Bila shaka hiyo ni jeuri iliyopindukia na hakuna atakayeivumilia. Ndipo hapo Mwenyezi Mungu (sw) akawapa Waislamu ruhusa ya kupigana. Ruhusa ya kwanza waliyopewa ilikuwa "Wameruhusiwa (kupigana) wale wanaopigwa, kwa sababu wamedhulumiwa. Na kwa yakini Mwenyezi Mungu ni muweza wa kuwasaidia ambao wametolewa majumbani mwao pasipo haki ila kwa sababu wanasema ‘Mola wetu ni Allah’ (Al Hajj 22:39-40)
Huo ukawa ndio mwanzo wa vita vya jihadi. Lakini msisitizo mkubwa waliowekewa ulikuwa wasipigane vita vya uvamizi bali vita vya kujihami. Na shahidi wa haya ni ile kauli ya Allah (sw) inayosema, "Na piganeni katika njia ya Mwenyezi Mungu na wale wanaokupigeni, wala msipindukie mipaka (mkawapiga wasiowapigeni). Kwani Mwenyezi Mungu hawapendi warukao mipaka" (Al Baqarah 2:190).
Ukichunguza utaona kila lnapotajwa neno jihadi katika Qur’an Tukufu au katika hadithi za Mtume (saw) basi huongezwa Fiy Sabilil Lahi. Maana yake jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu. Hii ni kwa ajili ya kuonyesha kuwa si lazima jihadi kila siku iwe ina maana ya vita.
Neno juhudi pamoja na kustahamili mashaka na taabu katika kufikia jihadi ni kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu kwa kustahili kila aina ya misukosuko inayoweza kumfika mtu.







0 comments:
Post a Comment