Familia hiyo ilikuwa ni familia duni sana hawakuweza kumudu ata chakula chao cha kila siku.
Waliishi ktk hali hiyo ya ufukara na umaskini uliopitiliza tokea wafunge ndoa wakivumiliana kwa hali hiyo waliyokuwa nayo.
Siku moja walipokuwa pmj kitandani mke akasema kumwambia mume wake.
"Mume wng hivi mussa a.s si ni nabii wa m/mungu tena anaongea nae.?"
Mume akamjibu mke wake kuwa ndivyo.
Mke akamwambia "ni kwa nn tusiende kwa nabii musaa a.s tumueleze juu ya hali yetu na ufukara tuliokuwa nao,
Kisha tumtake akatufikishie habari zetu hizi kwa m/mungu na atuombee ili nasi walau tuweze kumiliki chochote (kipato) ktk maisha yetu yaliyobakia!"
Mume akamuafiki mke wake kwa kumuambia kuwa ni mawazo mazuri.
Basi asubuhi kulipo pambazuka mume akatoka na kuelekea kwa nabii mussa a.s na kumuelezea juu ya hali yao
Na akimtaka akamfikishie habari hiyo kwa m/mungu na awaombee ili hali yao ibadilike walau nao waweze kuwa miongoni mwa waliokuwa navyo.
Nabii musaa a.s akatoka kwenda kuongea na mola wake juu ya hali ya familia ile.
M/mungu akamwambia nabii mussa a.s "ewe mussa a.s waambie kuwa nitawakunjulia rizki watakuwa na maisha mazuri,,,,,
Lakini kwa muda wa mwaka mmoja tu peke yake mwaka huo ukiisha watarudi tena ktk hali yao ya awali ya ufukara."
Nabii mussa a.s akarudi na kuwajulisha kuwa m/mungu amewakubalia maombi yao lkn atawaneemesha kwa muda wa mwaka mmoja tu.
Wale wanandoa wakazipokea taarifa hizo na baada ya muda mambo yakaanza kubadilika .
Ikawa wanapata kipato kwa njia ambayo wasiyoijua wala kutarajia.
Maisha yakaanza kubadilika na wakawa ni miongoni mwa watu waliokuwa navyo (matajiri).
Mke akasema kumwambia mume wake "mume wng hivi unakumbuka kuwa hali hii tuliyokuwa nayo na mali hizi ni kwa muda wa mwaka mmoja tu,,,,
Mwaka ukiisha tutarudi tena ktk hali yetu ile ile ya ufukara tuliyokuwa nayo?"
Mume akamuitikia kuwa ndio anakumbuka.
Mke akamwambia "kwa ajili hiyo ww unalionaje hili,,,,tunajenga umaarufu kwa pesa tuliyokuwa nayo na tunafanya starehe.
Mpaka watu wote wakajua juu ya utajiri wetu lkn mwaka ukiisha watu watakuwa wakisema kuwa tulikuwa matajiri lkn sasa ata ela ya kula hawana!"
Mume akamwambia mke wake "umenishauri jambo zuri ewe mke wng ni lazima tufanya jambo."
Wakaanza kujenga nymba sehemu za pembezoni mwa mabarabara za wasafiri.
Nyumba hizo wakizigawanya ktk sehemu saba tofauti tofauti.
Ktk nyumba hizo wakawaajiri watu wakiwahudumia wasafiri wanaopita sehemu hiyo kwa vyakula na vinywaji pasina malipo yoyote.
Wakawa wakishughulika na jambo hilo wakiwalisha wasafiri wapitao hapo usiku na mchana.
Siku miezi iliisha nabii mussa a.s akiwatazama juu ya hali waliyokuwa nayo pmj na utajiri wao.
Mwaka uliisha wakiwa ktk hali yao ile ile ya utajiri huku wakiendelea kuwahudumia watu.
Na hatimae ukaingia mwaka mwingine tena ilihali hali ya wale wanandoa ikiwa vile vile ya utajiri.
Nabii mussa a.s akashangaa na kwenda kumuuliza allah s,w
Nabii mussa akasema "ewe mola wangu ulisema kuwa utawapa mali kwa muda wa mwaka mmoja, na mwaka ukiisha watarudi ktk hali yao ya ufukara,
Ni kwa nn sasa mwaka umeisha na umeingia mwaka mwingine ilihali wale watu wakiwa ktk hali yao ile ile ya utajiri?"
M/mungu s,w akamjibu nabii mussa a.s akamwambia
"ewe mussa a.s mimi niliwafungulia mlango wng miongoni mwa milango yng ya rizki,
Wao wakafungua milango saba wakiwahudumia waja wng,
Ewe mussa a,s (kwa hilo walifanyalo) hivi ww ata huwaonei haya,
Ewe nabii mussa a.s hivi kiumbe anaweza kuwa ni mkarimu kunishinda mm mola wake.",,,,,,,,,,,,,,,,,,
Kuna msemo nausikia sana wakisema kuwa
" hakuna tajiri (aliyekuwa nacho) aliyewahi kufirisika kwa sababu ya kuwasaidia wengine. "
Mali inayotolewa kwa ajili ya kuwasaidia wengine m/mungu huizidisha mali hiyo kwa mtoaji.







0 comments:
Post a Comment